1 Chronicles 6:71-76


71 aWagershoni walipokea miji ifuatayo pamoja na maeneo yake ya malisho:
Katika nusu ya kabila la Manase:
walipewa Golani katika Bashani na pia Ashtarothi.

72 bKutoka kabila la Isakari
walipokea Kedeshi, Daberathi,
73Ramothi na Anemu, pamoja na maeneo yake ya malisho.

74 cKutoka kabila la Asheri
walipokea Mashali, Abdoni,
75 dHukoki na Rehobu, pamoja na maeneo yake ya malisho.

76 Kutoka kabila la Naftali
walipokea Kedeshi katika Galilaya, Hamoni na Kiriathaimu pamoja na maeneo yake ya malisho.

Copyright information for SwhKC